Sunday, March 5, 2017

MANENO LYRICS AND TRANSLATION BY REBEKAH DAWN


Wakati mwingine nikiketi kukuimbia mie
(Sometimes when i sing for you)
Huwa nalemewa kupata maneno yanayoshimiri
(i lack the best words to define you)
Ni kama mtoto mchanga anapojaribu kueleza ukubwa wa sayari
(its like a child explaining how big the universe is)
Ni kama kidege kinapojaribu kueleza upana wa mbingu
(like a bird trying to explain how big the sky is)
Ni kama changarawe kujaribu kueleza ukubwa wa bahari
(like sand trying to explain how bog the ocean is)

Ukweli ni kwamba maneno yangu hayatoshi, hayawezi kueleza
my words ain't enough to explain)
Hivyo daima na milele siku zote za maisha yangu
(for the rest of my life)
Nitatafuta kukuimbia maneno yanayokufaa
(i will sing the best words for you)

Wakati mwingine nikiketi kukuimbia mie
(Sometimes when i sing for you)
Huwa nalemewa kupata maneno yanayoshimiri
(i lack the best words to define you)
Ni kama tone la maji kujaribu kueleza mfuriko wa mvua
(like a raindrop trying to explain the downfall of rains)
Ni kama wapendanao kujaribu kueleza fumbo la penzi
(like lovers trying to explain the mysery of love)
Ni kama mshumaa kujaribu kueleza kung’aa kwa jua
(like a candle trying to explain the brightness of sun)

Ukweli ni kwamba maneno yangu hayatoshi, hayawezi kueleza
(my words ain't enough to explain)
Hivyo daima na milele siku zote za maisha yangu
(for the rest of my life)
Nitatafuta kukuimbia maneno yanayokufaa
(i will sing the best words for you)


Ni kama jiwe linapojaribu kueleza urefu wa mlima
(like a stone trying to explain the height of a mountain)
Ni kama sheha shupavu kujaribu kueleza hadithi zote za jadi
(like a storysteller explaining all long time stories)
Ni kama mwenye dhambi kujaribu kueleza neema ya msamaha
(like a sinner explaining the grace of forgiveness)

Ukweli ni kwamba maneno yangu hayatoshi, hayawezi kueleza
(my words ain't enough to explain)
Hivyo daima na milele siku zote za maisha yangu
(for the rest of my life)
Nitatafuta kukuimbia, nitatafuta kukuimbia
Maneno yanaykuofaa
(i will sing the best words for you)


No comments: