Friday, December 4, 2015

WARANDARANDA LYRICS BY CHRISTINA SHUSHO



Verse1
Yalinenwa na manabii  kale,
Kwamba atazaliwa,mwanamume,
na ufalme utakuwa begani mwake
Ataitwa Emmanuel japo miaka ilipita,
Lakini neno lilitimia,
(salamu maria, umejaa neema,
bwana yu nawe,
umebarikiwa kuliko wanawake wote)x2
wapi yusufu, wa ukoo wa daudi,
unabii umetimia kwako,

(refrain)
Warandaranda mbao tu,(yusufu we)
usiku mchana,we mbao,(wewe yusufu)
Warandaranda mbao tu,(kumekucha yusufu)
yusufu fundi wa mbao,x2


verse2
(nyumba zimejaa ,za wageni zimejaa,
yusufu zimejaa,Bethlehem kumejaa)x2
ni wakati wa *sensa ,(kumejaa)
wageni ni wengi,(kumejaa)x2)x2

(refrain)
Verse3
Mioyo imejaa mambo,
Masumbufu ya maisha yakutesa,
Mpaka umesahau ahadi za mungu,
Ata usiku uwe mrefu kutakucha,
Fungua moyo azaliwe kwako,
Akizaliwa atafanya mambo mapya,
Neno lake halirudi bure,
Akiahidi lazima atimize,
Wacha kuranda mbao ,we kuranda mbao
Wewe,kuranda mbao,


(refrain)

No comments: