Showing posts with label AOCC RWANDA. Show all posts
Showing posts with label AOCC RWANDA. Show all posts

Tuesday, April 7, 2015

SIKU ZA KILIO ZIMEPITA LYRICS BY AMBASSADORS OF CHRIST CHOIR RWANDA 2015








Sauti ilisikika mjini ramah,
Kilio na maombolezo mengi,
Reali akiwalilia watoto wake,
Lakini hakutaka kufarijiwa kwa kuwa hawapo tena

Bwana asema hebu zuia sauti yako, usilie mama,
Na macho yako, yasitoke machozi , tulia eeh jipe moyo.
Maana  kazi yako itapata dhawabu,
Na kwa nguvu mpya, nguvu mpya utainuliwa tena,

Wakati tulio nao, si wa kuomboleza tena,
Siku za kilio zimepita zimekwisha ,  aha
Sasa twasonga tena, mbele kwa kazi yake bwana,
Matukio kamwe hayatatukatisha tamaa ,
Na tutaweza yote,kwa jina lake mwenye nguvu,
Na kwa mkono wake yeye mwenyewe atatuongoza

Twatiwa nguvu kwa neno lake bwana mungu,
Asemapo baada ya hayo yote nitarejea,
Nami nitaijenga tena nyumba yake daudi ,iliyoanguka,
Nitajenga tena maanguko yake , nitaisimamisha,

Kwa ajili yake bwana twaweza kuuwawa mchana , usiku kucha,
Twahesabiwa kuwa kama kondoo wasubirio kuchinjwa,
Lakini katika mambo hayo yote tumeshinda na zaidi ya kushinda kwa yeye aliyetupenda jina lake lisifiwe milele,
Baada ya siku hizo za kupigwa vikali,
Kama alivyoahidi nguvu mpya, ametupatia tena

Wakati tulio nao, si wa kuomboleza tena,
Siku za kilio zimepita zimekwisha ,  aha
Sasa twasonga tena, mbele kwa kazi yake bwana,
Matukio kamwe hayatatukatisha tamaa ,
Na tutaweza yote,kwa jina lake mwenye nguvu,
Na kwa mkono wake yeye mwenyewe atatuongoza x3



KWETU PAZURI LYRICS BY AMBASSADORS OF CHRIST CHOIR RWANDA


Ninayo hamu kurudi nyumbani
Nyumbani kwetu ambapo hatutatengana
hapo nyumbani kwetu hakuna makaburi
Wala hakuna vyandarua maana hakuna malaria
Kwetu pazuri ni pazuri nakuambia
Najua nawe ndugu yangu unayo hamu kufika huko


kwetu pazuri nimeshapakumbuka
Ninayo hamu kuishi na mwokozi wangu
Kwa amani na furaha tena ya ajabu
Sipati picha kwa watakaofika kwetu mbinguni*2


Hii dunia imejaa shida kama hujui nenda hospital kaone
Lakini kwetu hakuna fani ya tabibu
Watakatifu watachuma majani ya mti wa uzima wawe na afya
Hawataugua magonjwa tabu tutaziacha zote hapa duniani

Mpendwa njoo, turudi nyumbani
Asubuhi yaja tuyakimbie ya dunia
Atayekosa hapo kweli ni hasara
Aya matatizo ni mitego ya shetani
Hili tushindwe kufika nyumbani kwetu pazuri
Lakini kwa jina jina la Yesu tumemshinda tunaenda